16. Tunakuamkia Yesu

1 Tunakuamkia Yesu
tunakupa pongezi.
Umezaliwa kikiwa,
malaika wakuabudu,
Uwe nasi!

2 Mwana wa Mungu wa pekee,
yeye ni mgeni wetu.
Anajiunga na sisi
Mfalme wa kale na kale!
Uwe nasi!

3 Ashikaye ulimwengu
ashikwa na Maria!
Ni mtoto mdogo na mchanga!
Tena ni Bwana wa mbingu!
Uwe nasi!

4 Nuru ya milele aja
kuleta mwanga wake.
Aondoa giza lote;
tuwe watoto wa mwanga.
Uwe nasi!

5 Kwetu akawa maskini
kwa kutuhurumia,
tupate mali ya mbingu,
tuwe watoto wa Mungu.
Uwe nasi!

6 Amefanya haya yote
kwa kuwa atupenda.
Kwa hiyo fuahini tu
na tumshukuru daima!
Uwe nasi!

Text Information
First Line: Tunakuamkia Yesu
Title: Tunakuamkia Yesu
German Title: Gelobet seist du, Jesu Christ
Author: M. Luther, 1483-1546
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kuzaliwa kwa Yesu
Notes: Sauti na wimbo: Gelobet seist du, Jesu Christ, Asili: J. Walther, Wittenberg, 1524, Posaunen Buch, Erster Band #15, Lutheran Book of Worship #48
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us