Text: | Mungu tusaidie |
1 Mungu tusaidie,
Sisi tunaangamia.
Nchi imeharibika
Na mwovu wake Shetani.
Refrain:
Kweli kweli ndiye Yesu
Aliyewambwa mtini
Penye mlima wa Golgotha
Aokoe wenye dhambi.
2 Kaonyesha huruma,
Wayuda wakasumbua.
Wakampiga makofi,
Pilato aliamua. [Refrain]
3 Yesu mwenye upendo
Alikubali kuuawa,
Damu ilimwagika
Ili sisi tuokoke. [Refrain]
4 Pale msalabani,
Bwana Yesu aliteswa
Mzigo wa dhambi zetu
Ulimwangukia yeye. [Refrain]
5 Sote na tukumbuke,
Kifo cha Mwokozi wetu.
Alisema ya kwamba
Jililieni wenyewe. [Refrain]
6 Habari zilisemwa,
Mahali hapa hayupo,
Ona alipokuwa,
Jiwe limeondolewa. [Refrain]
7 Ni ajabu kabisa
Wingu kuja kumpokea.
Habari ilisema
Yesu atarudi tena. [Refrain]
Text Information | |
---|---|
First Line: | Mungu tusaidie |
Title: | Mungu tusaidie |
Refrain First Line: | Kweli kweli ndiye Yesu |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Kuteswa na kufa kwa Yesu |
Notes: | Suati: Kinyakyusa |