Instance Results

Topics:epifania
In:instances

Planning worship? Check out our sister site, ZeteoSearch.org, for 20+ additional resources related to your search.
Showing 61 - 70 of 244Results Per Page: 102050
Page scan

Mmoja ndiye tumpendaye

Author: A. Knapp, 1798-1834 Hymnal: Mwimbieni Bwana #54 (1988) Topics: Epifania, Mission Languages: Swahili
TextPage scan

Mmoja ni Mfalme

Author: J. L. K. Allendorf Hymnal: Mwimbieni Bwana #55 (1988) Topics: Epifania, Mission First Line: Mmoja ni mfalme shujaa Lyrics: 1 Mmoja ni mfalme shujaa, ni mshindaji! Enyi adui, kimbieni tu! Nawe Sioni uone furaha ukapumzishe kabisa moyo: Uzima, utengemano, furaha ndizo Mwokozi atakazokupa. 2 Twende kuonja maji ya uzima tunayopewa na Bwana Yesu, aliyesema "Njooni kwangu wote, nitapumzisha mioyo yenu!" Nyweni, wapenzi, katika kisima chenye wokovu wa wenye huzuni. 3 Mfalme wa mbingu ataka kuwapa kilemba kizuri cha urembo, awawekea viti vya milele, heshima hiyo ni ya kushinda. Vumilieni taabu na shida: Yesu mwenyewe ni tuzo la vita. 4 Nguvu, ujuzi, heshima na sifa ni sake Mungu na Mwana wake. Nami nataka kufika mbinguni! Nifunguliwe mafungo yangu! Mwenye upendo atasikia. Wenye uzima wanamsifu Mungu. Languages: Swahili
TextPage scan

Nani mpenzi wangu mkuu?

Author: J. C. Schwedler, 1672-1730 Hymnal: Mwimbieni Bwana #56 (1988) Topics: Epifania, Mission Lyrics: 1 Nani mpenzi wangu mkuu? Nani ninayemsifu? Nani ninayemjua? Nani ninayempenda? Ndiye Yesu Mwokozi. Ndiye Yesu Mwokozi. 2 Nani nimtegemee, anipaye moyo mkuu? Nani aondoaye makosa, shida zangu? Ndiye Yesu Mwokozi. Ndiye Yesu Mwokozi. 3 Nani anayenipa nguvu nyingi za roho? Nani anifanyaye mwenye haki kwa Mungu. Ndiye Yesu Mwokozi. Ndiye Yesu Mwokozi. 4 Nani mwenye faraja, nikiona huzuni? Nani atulizaye moyo wenye taabu? Ndiye Yesu Mwokozi. Ndiye Yesu Mwokozi. 5 Nani azishindaye hata nguvu za kufa? Nani anipeleke baadaye kwake Mungu? Ndiye Yesu Mwokozi. Ndiye Yesu Mwokozi. Languages: Swahili
TextPage scan

Del Oriente somos los tres

Author: John Henry Hopkins, Jr. (estadounidense, 1820-1891); Effie Chastain de Naylor (estadounidense, 1899-1983) Hymnal: Las Voces del Camino #57 (2009) Topics: Epifania Refrain First Line: ¡Oh, astro de subline ardor Lyrics: 1 Del Oriente somos tres, cabalgamos hasta Belén, que ha nacido el prometido, príncipe de Israel. Estribillo: ¡Oh, astro de sublime ardor, de divino resplandor! Nuncio bello, tus destellos nos guíarán con tu fulgor. 2 Del lucero vamos en pos, nos conduce al hijo de Dios; yo le ofrezco dulce incienso, le rindo adoración. [Estribillo] 3 Ha venido al mundo la luz; mirra yo le ofrezco a Jesús, mirra pura, amargura, símbolo de la cruz. [Estribillo] 4 Oro traigo para el rey que ha nacido aquí en Belén; rey excelso, rey eterno, del mundo sumo bien. [Estribillo] Languages: Spanish Tune Title: KINGS OF ORIENT
TextPage scan

Kazi ni yako Bwanangu

Author: S. Preiswerk; F. v. Zaremba, 1794-1874 Hymnal: Mwimbieni Bwana #58 (1988) Topics: Epifania, Mission Lyrics: 1 Kazi ni yako Bwanangu tunayoifanya; hakuna anayeweza kuvunja kazi hii. Ni kama punje ya mbegu ikiwa ndani ya mchanga, inakufa kwa kuoza; na hapo yabadilika, inaota, yakua na kuzaa. 2 Yesu, umeteswa kwanza, halafu umepaa. Nao wakufuatao wanateswa vivyo. Twaomba tusaidie nasi tushike njia hii, kwa kufa kwako na sisi tunatoka kaburini. Tuongoze, tufike mbinguni. 3 Bwana wewe umekufa kwa ajili yetu. Ukaweka ufufuo ulipofufuka. Twaomba: Tuma mitume, wajulishe jina lako mpaka mwisho wa dunia. Utukabali na sisi kwa kazi hii, tutume, twakutii! Languages: Swahili
TextPage scan

Ufalme wa Mungu

Author: C. B. Garve, 1763-1841 Hymnal: Mwimbieni Bwana #59 (1988) Topics: Epifania, Mission Lyrics: 1 Ufalme wa Mungu uenee popote! Nguvu yako iokoe wakaao gizani. Uondoe woga wote, ukawape watu uzima, ufalme wa Mungu. 2 Ushinde upesi! Uharibu ufalme wa Shetani duniani, ndiye mfalme wa giza. Nawe utamshinda yeye, kwani una nguvu ya Mungu. Ushinde upesi! 3 U Shujaa wa Mungu! Kwa rehema ya Bwana urudishe watu kwako, wapendane kwa moyo, wawe raia wako pote. Ndipo utatukuzwa sana! U shujaa wa Mungu! 4 Duniani popote jina lako livume nguvu zako zisifiwe na makabila yote, uliowatengemaza, mpaka utakapotawala duniani popote! 5 Shikeni amri hii: Tangazeni popote kwa makabila yoyote neno lenye furaha, wapate kuokolewa. Yesu aliyotuagiza. Shikena amri hii! 6 Sifuni rehema ya kuokoa watu! Tikimtumikia Bwana, azibariki kazi zote za mikono yetu; amani kuu iwe kwetu. Sifuni rehema! Languages: Swahili
TextPage scan

Sifuni nyote huruma

Author: M. A. v. Löwenstern, 1594-1648 Hymnal: Mwimbieni Bwana #60 (1988) Topics: Epifania, Mission First Line: Sifuni nyote huruma ya Mungu Lyrics: 1 Sifuni nyote huruma ya Mungu kwa nyimbo nzuri, umati wa Yesu! Atualika furahani: Msifuni Bwana kwa neema yake! Msifuni Bwana kwa neema yake! 2 Yeye ni mfalme anayetawala; viumbe vyote vinamtumikia, hata malaika wamwabudu, wanamwimbia kwa sauti nzuri, wanamwimbia kwa sauti nzuri. 3 Enyi mataifa, hofu iacheni! Njooni kwa Yesu, mchunga kondoo mwema. Sikilizeni neno lake: Atukomboa kwa ufa kwake, Atukomboa kwa ufa kwake. 4 Awapa watu chakula chochote, atushibisha kama baba mzuri, aleta jua hata mvua, atubariki kwa wema wake, atubariki kwa wema wake. 5 Sifuni nyote huruma ya Mungu kwa nyimbo nzuri, umati wa Yesu! Sasa huzuni twaishinda: Msifuni Bwana kwa neema yake! Msifuni Bwana kwa neema yake! Languages: Swahili
TextPage scan

Uamke kwetu tena Roho

Author: K. H. v. Bogatzky, 1690-1774 Hymnal: Mwimbieni Bwana #61 (1988) Topics: Epifania, Mission Lyrics: 1 Uamke kwetu tena Roho ya mashahidi wale wa kwanza, waliokesha siku zote, waliomshinda yule adui, wakihubiri neno la Yesu kwa watu wa ulimwengu wote. 2 Uwashe moto wa upendo, uendelee pote kuwaka. Peleka watu mavunoni, wanaofanya kazi kwa bidii. Bwana mwenye mavuno, tazama: Watenda kazi yako ni haba. 3 Mwanao ametuaqiza kuomba hivi kwa jina lake, na sisi wanafunzi wake, twashika neno lake kwa bidii. Twaomba hivi kwa moyo wote. Ee Bwana usikie, ufanye! 4 Utame watu wengi sana, walitangazi neno kwa nguvu. Usaidie tuokoe, ufalme wa Shetani uishe. Usimamishe, Bwana wa mbingu, ufalme wako ulimwenguni! 5 Uteme mwema na uende mahali popote huku nchini, wamizimu na waingie kundini mwako mwa wateule. Amsha nao Waisraeli na Waislamu waje, wakutii. Languages: Swahili
TextPage scan

Yesu, mfalme, utiishe

Author: Hajulikani Hymnal: Mwimbieni Bwana #62 (1988) Topics: Epifania, Mission Lyrics: Yesu, mfalme, utiishe upesi ulimwengu wote, viumbe vyote vikutii. Ubariki neno lako, utoe roho wa uzima, uamshe wanaolala. Bwana, usikie tunavyokuomba. Amin, Amin! Tutaimba Haleluya na nyimbo za kukusifu. Languages: Swahili
TextPage scan

Yesu ni mponya

Author: J. L. K. Allendorf Hymnal: Mwimbieni Bwana #64 (1988) Topics: Epifania, Mission Lyrics: 1 Yesu ni mponya, aleta furaha! Mwanzo na mwisho wa vyote ndiye. Mwana Adamu na Mungu wa kweli ametujia atubariki. Mbingu, dunia, toeni habari: Yesu ni mponya, aleta furaha! 2 Yesu ni mponya, aleta wokovu! Sikilizeni habari njema! Sisi tulipomwacha Mungu wetu akaturudisha tena kwake. Ametufanya watoto wa Mungu. Yesu ni mponya, aleta wokovu. 3 Yesu ni mponya, aleta uzima! Kamba za kufa zimekatika. Mwana wa Mungu kamshinda Shetani, awakomboe watumwa wake, amewapata, kawapa uhuru. Yesu ni mponya, aleta uzima. 4 Yesu ni mponya, mchungaji wa kweli, anayelisha vizuri kondoo. Wote walio mbali awaita, awarudishe kundini mwake. Awakomboa kondoo kufani: Yesu ni mponya, mchungaji wa kweli. 5 Yesu ni mponya na mfalme wa enzi! Mbingu zimsifu na watu wamtii. Anageuza mioyo ya watu, hata na sisi na tumpe yetu, kwani apenda kutupa uzima. Yesu ni mponya na Mfalme wa enzi! 6 Yesu ni mponya na mwenye upendo! Anatupenda kwa moyo wote. Yeye mwenyewe upendo wa kweli, aliyekufa kwa kutupenda. Nasi tumpende kwa nguvu ya roho! Yesu ni mponya na mwenye upendo! Languages: Swahili

Pages


Export as CSV