Ewe Bwana ndiwe Mchunga wangu mwema

Ewe Bwana ndiwe

Author: Mudimi Ntandu
Published in 1 hymnal

Representative Text

1 Ewe Bwana ndiwe
mchunga wangu mwema.
Sitapungukiwa na kitu,
Kwani u pamoja nami.

2 Wanilaza kwenye
malisho tele;
Wanitangulia vizuri,
Kwani wanipenda sana.

3 Nafsi yangu
imehuishwa nawe,
Na kuongozwa kwa haki,
Kwa ajili ya jina lako.

4 Nikipitia hata
bonde la mauti,
Sitaogopa mabaya,
Kwani Wee u gongo langu.

5 Umeandaa meza
mbele yangu mimi,
Ili na watesi waone,
Kwamba ndiwe
mwenye neema.

6 Kichwa changu
kimepakwa na mafuta.
Kombe langu linafuika;
Haya umefanya yote.

7 Wema wako
umenifuata hasa.
Nami nitaishi na Wewe,
Kwako, Bwana siku zote.

Source: Mwimbieni Bwana: msifuni Mungu, mfalme wa mbingu na nchi! #273

Author: Mudimi Ntandu

(no biographical information available about Mudimi Ntandu.) Go to person page >

Text Information

First Line: Ewe Bwana ndiwe
Title: Ewe Bwana ndiwe Mchunga wangu mwema
Author: Mudimi Ntandu
Language: Swahili
Notes: Asili: Zaburi 23, Sauti Kinyaturu, Tumshangilies Mungu #98

Instances

Instances (1 - 1 of 1)
Text

Mwimbieni Bwana #273

Suggestions or corrections? Contact us