1 Mungu kanilinda mimi
kwa wema mpaka leo.
Alinda mwili na roho
usiku hata mchana.
Aniongoza kila saa,
apenda kunibariki
na kunisaidia.
2 Ninakushukuru Mungu
sababu ya rehema,
uliyonifanyizia
Bwanangu siku zote.
Ninakumbuka daima
mambo unitendeayo,
ukanisaidia.
3 Uzidi kunibariki,
kwa wema wako Bwana.
Nisaidie kila saa
na mahali popote.
Nimshike Yesu Mwokozi,
hata na siku ya kufa
nipate mwisho mwema.
Text Information | |
---|---|
First Line: | Mungu kanilinda mimi |
Title: | Mungu kanilinda mimi |
German Title: | Dis hierher hat mich Gott gebracht |
Author: | A. J. v Schwarzburg Rudolstadt, 1637-1708 |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Kumtambikia Mungu: Sikukuu za Wakristo |
Notes: | Sauti: Bis hierher hat mich Gott gebracht, Posaunen Buch, Erster Band #114, Nyimbo za Kikristo #182 |