Instance Results

Topics:epifania
In:instances

Planning worship? Check out our sister site, ZeteoSearch.org, for 20+ additional resources related to your search.
Showing 71 - 80 of 244Results Per Page: 102050
TextPage scan

Mfalme ni Yesu pekee

Author: P. F. Hiller, 1699-1769 Hymnal: Mwimbieni Bwana #65 (1988) Topics: Epifania, Mission Lyrics: 1 Mfalme ni Yesu pekee, wote wanamwangukia, watawalishwa na Mungu. Ndimi zote ziungame Yesu ni mfalme pekee, atukuzwe popote. 2 Mfalme mkubwa, watu wako wakutii, wanakusifu. Yesu apita wafalme, yeye ndiye mkubwa sana, apenda kuwakomboa, kwani ndiye Mwokozi. 3 Enyi watu mpeni mioyo, mnaohuzunika njooni; wakiwa semeni naye, kwani vyote aviweza. Awagawia uzima wanaomngoja yeye. 4 Kama wataka uzima, nenda kwake, acha soni, yeye anakungojea. Amejitoa mwenyewe, wewe upate kurithi, mbingu ni yako sasa. 5 Nimsifuje Yesu Kristo mimi vumbi, mimi jivu? Nasema: Nitamtangaza Kristo Yesu ndiye Bwana! Na tumpende, tumheshimu sifa zote zampasa. Languages: Swahili
TextPage scan

Nyesha mvua

Author: R. Amstein, 1846-1923 Hymnal: Mwimbieni Bwana #66 (1988) Topics: Epifania, Mission First Line: Nyesha mvua, nyesha mvua Lyrics: 1 Nyesha mvua, nyesha mvua, wewe Roho wa Baba, nchi kavu ikanyweshwe, imsifu Mungu wetu! 2 Vuma sana, vuma sana, Roho mwenye uzima, tulio na usingizi utuamshe kwa mkono! 3 Toa mwanga, toa mwanga, Roho kwani unang'aa wewe ushinde usiku tusikae na giza. 4 Sikiliza, sikiliza, wewe mfalme wa mbingu! Tuma Roho wako kwetu, kote kuwe na upya! Languages: Swahili
Page scan

Nitakutukuza

Author: G. Knak Hymnal: Mwimbieni Bwana #67 (1988) Topics: Epifania, Mission Languages: Swahili
TextPage scan

Wito waja

Author: W. Hellemann Hymnal: Mwimbieni Bwana #68 (1988) Topics: Epifania, Mission First Line: Wito waja, kwa nchi zote Lyrics: 1 Wito waja, kwa nchi zote wapi washindi wa Yesu watakaomfuata kweli? Sisi tujitie kwake! Mkubwa nani? tushikane naye mfalme, tupatane, tumfuate! 2 Ana ufalme tangu kale, nchi hata mbingu ni zake. Atuelekeza juu kwake, hatahukumiwa tena. Mkubwa nani? tushikane naye mfalme, tupatane, tumfuate! 3 Tutangaze utume mwema kwa makabila ya kwetu, na tuseme pasipo woga tuyaonayo kwa Yesu. Mkubwa nani? tushikane naye mfalme, tupatane, tumfuate! 4 Haya jamaa tuwe tayari sisi watumishi wake, yeye ni mfalme wa majeshi miili na mioyo ni yake. Mkubwa nani? tushikane naye mfalme, tupatane, tumfuate! Languages: Swahili
Text

Twende vitani

Author: C. G. Bath, 1799-1862 Hymnal: Mwimbieni Bwana #69 (1988) Topics: Epifania, Mission Lyrics: 1 Twende vitani vitakatifu, zitakapokuja shida na taabu. Ngurumo zivume kutia woga. Mwiteni Mwokozi! Yesu ni mwanga. 2 Ingawa giza lawafunika, na raha yenu ikizimika, na nguvu za mwovu hazina mpaka. Mwiteni Mwokozi! Yesu ni mwanga. 3 Shetani aje, akijaribu kuvunja kazi na kuharibu hila zake zote na zitakwisha. Mwiteni Mwokozi! Yesu ni mwanga. Languages: Swahili

Wajibu mwema watoka kwako

Author: Enock Kalembo Hymnal: Mwimbieni Bwana #70 (1988) Topics: Epifania, Mission Languages: Swahili
TextPage scan

Tumesikia mbiu

Author: Priscilla Owens Hymnal: Mwimbieni Bwana #71 (1988) Topics: Epifania, Mission Lyrics: 1 Tumesikia mbiu: Yesu, lo! aponya; Itangazeni kote, Yesu, lo! aponya. Tiini amri hiyo: Nchini na baharini, Enezeni mbiu hii: Yesu lo! aponya. 2 Imbeni na vitani: Yesu, lo! aponya; Kwa nguvu ya Mkombozi, Yesu lo! aponya. Imbeni wenye shida, Unapoumwa moyo, Na kaburini imba: Yesu lo! aponya. 3 Mawimbini ienee: Yesu lo! aponya: Wenye dhambi jueni: Yesu lo! aponya Visiwa na viimbe, Vilindi itikeni, Nchi shangilieni: Yesu lo! aponya. 4 Upepo utangaze: Yesu lo! aponya; Mataifa yashangaa: Yesu lo! aponya Milimani bondeni, Sauti isikike Ya wimbo wa washindi: Yesu lo! aponya. Languages: Swahili
TextPage scan

Ni ujumbe wa Bwana

Author: W. A. Ogden Hymnal: Mwimbieni Bwana #72 (1988) Topics: Epifania, Mission Refrain First Line: Tazama! Ishi sasa! Lyrics: 1 Ni ujumbe wa Bwana, Haleluya! Wa maisha ya daima. Amesema mwenyewe, Haleluya! Utaishi ukitazama. Refrain: Tazama! Ishi sasa! Kumtazama Yesu. Amesema mwenyewe, Haleluya! Utaishi ukitazama. 2 Ni ujumbe wa wema, Haleluya! Nawe shika, rafiki yangu. Ni habari ya raha, Haleluya! Mwenye kuisema ni Mungu. [Refrain] 3 Uzima wa daima, Haleluya! Kwake Yesu utauona. Ukimtazama tu, Haleluya! Wokovu pekee wa Bwana. [Refrain] Languages: Swahili
TextPage scan

Ni wako wewe, nimekujua

Author: Fanny Crosby Hymnal: Mwimbieni Bwana #73 (1988) Topics: Epifania, Mission Refrain First Line: Bwana vuta, vuta Lyrics: 1 Ni wako wewe, nimekujua Na umeniambia, Lakini Bwana, nataka kwako Nizidi kusogea. Refrain: Bwana vuta, vuta nije nisogee sana, kwako mtini. Bwana vuta, vuta, Nije nisogee, Pa damu ya thamani. 2 Niweke sasa nikatumike Kwa nguvu za neema; Uyapendayo nami nipende, Nizidi kukwandama. [Refrain] 3 Nina furaha tele kila saa Nizungumzapo kwako. Nikuombapo nami napata Kujua nia yako. [Refrain] 4 Mapenzi yako hayapimiki, Ila ng'ambo yaliko. Anasa pia sitazijua, Bila kufika kwako. [Refrain] Languages: Swahili
Page scan

Mikononi mwa mitume

Author: Mch. Sila Msangi Hymnal: Mwimbieni Bwana #74 (1988) Topics: Epifania, Mission Refrain First Line: Nenda, nenda Languages: Swahili

Pages


Export as CSV