17. Tuimbe na kusifu

1 Tuimbe na kusifu
kwa nyimbo za furaha:
Yesu Bwana wetu
amezaliwa leo
zizini Betlehemu,
furaha ya mioto.
Mponya na Mwokozi,
tunakusifu.

2 Nakutamani sana,
uliyetoka juu.
Ee Mowokozi mwema
tuliza moyo wangu,
unipe neema yako,
Mtoto wa huruma.
Univute juu, univute juu.

3 Rehema zake Mungu
ni nyingi, alimtuma
Mwana wake Yesu,
awakomboe watu,
atufanyie njia,
tufike tena kwetu.
Kwetu ni kwa Mungu,
kwetu kwa Mungu.

4 Na watu wakaao
katika giza wote
wanakungojea
wewe Mowokozi wetu,
na kukufurahia
uliyetukomboa.
Yesu Bwana wetu
twakutukuza.

Text Information
First Line: Tuimbe na kusifu
Title: Tuimbe na kusifu
German Title: Nun singet und seid froh
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kuzaliwa kwa Yesu
Notes: Sauti: In dulci jubilo, Asili: Karne 1500, Posaunen Buch, Erster Band #231, Lutheran Book of Worship #55
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us